Timu ya Soka ya Kengold ya mkoani Mbeya katika wilaya ya Chunya inayomilikiwa na Mwekezaji Mzawa wa Madini ya Dhahabu na Mmiliki wa Shule ya Pre & Primary School ya Kengold ya Wilayani aitwaye Kenneth inazidi kung'ang'ania namba moja ikijikusanyia pointi 39 ikiiacha timu ya soka ya Pamba ya mkoani Mwanza kwa pointi 2 yenye pointi 37 huku kila timu ikiwa imecheza michezo 17. Na kwenye msimamo huo timu ya zamani ya Afisa Habari Masau Bwire Ruvu Shooting ikiburuza mkia ikiwa na pointi 3 tu na haijabahatika kushinda mchezo hata mmoja katika michezo hiyo 17.
Unafikiri timu ya soka ya Kengold itasalia hapo juu mpaka mwisho wa michuano au ni nguvu ya soda? Toa maoni yako.