NITAKUUA MWENYEWE - 20 (Mtunzi: Sultan Uwezo)

 


NITAKUUA MWENYEWE - 20

sultanuwezotz.blogspot.com 


"Kwa-ni-ni m-nat-ufa-nyia hiiiiviiiii?"

Robinson aliongea kwa taabu sana kwani muda alikuwa akitokwa na damu kila sehemu ilipitiwa na mingumi ya wale majitu.

"Tuk...o wap.."

Jackline alishindwa kumalizia sentensi akazimia tena na alikuwa hatamaniki hata kidogo kwani nguo zake tu zilikuwa kama vile zilikuwa zikitobolewa na misumari upande wa Jasmine na mdogo wake ndiyo kabisa hawakuwa wanajua kinachoendelea walikuwa wamezimia muda mrefu.

"Mtajuta kuitambua Kambi hii kichapo kidogo tu mnazimia? James waondoe wenge hao haraka."

Mzee Bruno aliagiza.

James alichukua lile kontena lenye maji ya barafu na kuwamwagia kila mmoja. Walizinduka lakini walikuwa walikuwa bado wanamaumivu makali mwilini kwani kila mmoja alikuwa akilalamika kivyake.

"Bila shaka bado hawajitambui vizuri hebu niletee lile beseni niwaweke nembo ambayo wataikumbuka maishani mwao."

Alisogezewa beseni lile ambalo lilikuwa na visu ndani yake na kisha kuanza kuwapiga chapa ya moto kwa kila mmoja.

"Mamaaaaa nakufaa mzee mbona unatufanyia hivyo?"

Robinson alilalamika baada ya kisu cha moto kupita kifuani kwake.

"Kumbe mnaweza kuongea vizuri ee mbona mwanzo mlikuwa mnakatakata maneno?"

"Nakuahidi mzee tukitoka kwenye jengo hili tutakachokifanya Ulimwengu wote utatushangaa."

Jackline aliongea huku kisu cha moto kikikatisha taratibu mgongoni lakini badala ya kulia kama wenzake yeye alimkazia macho mzee Bruno na kuongea hayo na mwisho alimtemea mate usoni yenye mchanganyiko na damu.

" Unanifanyia nini wewe binti? Kumbe hunijui eee."

Mzee Bruno alimuwakia baada ya tendo la kutemewa mate.

"Thubutuuuu kumbe hunijui wewe mzee, sasa ukitaka kujua mimi ni wa namna gani fungua hii minyororo nikuoneshe na kwa kuanza naanza na hawa wakosa sura."

Jackline alichafukwa kiasi cha kuwashangaza wenzake hasa Jasmine ambaye muda wote aliamini yeye ni zaidi ya wote kutokana na mafunzo aliyopitia na muda wote kutokana na ukimya wa Jackline alijua hajui chochote.

" Jackline achana na mawazo hayo kumbuka kuwa tuko gizani na hatujui itakuja nuru itakuja saa ngapi tuwe wapole love."

Robinson aliona amshauri mpenzi wake kwani anamfahamu akipaniaga jambo huwa harudi nyuma.

"Muache yeye si ameamua kuvimba kifua mbele ya wanaume sasa ngoja apewe somo. James mfungulie minyororo hiyo huyo bwege kisha kaandaeni lile eneo la machinjio."

Mzee Bruno Gautier alitoa maagizo ambayo yaliwatisha wakina Jasmine, Jessica pamoja na Robinson ambao walianza kulia wakimuonea huruma mwenzao. 

"Kama ulivyoagiza bosi."

James Martin aliitikia maagizo ya mkuu wake na kumfuata Jackline kumfungua minyororo, lakini kabla hajafanya hivyo Robinson alimrukia James na kumpiga na minyororo ya mkononi.

"Unanigonga na minyororo ee unataka shida brother?"

"Hapana ni bahati mbaya tu ila nilitaka kukuzuia usimfungue huyo bahati mbaya minyororo ikatangulia please nisamehe."

Haikusaidia kitu kwani James alimtandika teke la tumboni lililopelekea Robinson kuangukia kwenye magunia ya nafaka.

"Jiangalie kijana utakufa kabla ya wakati wako ohhohh shauri yako."

"Ha ha ha ha ha safi sana mjeshi wangu ndiyo maana kila siku napenda kukupandisha mavyeo kama yote fanya kazi yako achana na kelele za huyo pimbi."

"Sawa mkuu."

"Jackline please usifanye hivyo tutashindwa kufanikisha zoezi letu."

Jasmine alimnong'oneza Jackline sikioni akiamini atamuelewa lakini haikuwa hivyo.

"Jasmine wacha niwaoneshe kazi hawa washenzi maana tukiwakalia kimya watatupanda kichwani."

Sauti ile ya juu ilimfanya Jasmine ajivute pembeni na kubaki mtazamaji tu kama ambavyo Jessica alifanya.

Baada ya kufunguliwa tu Jackline alisimama kwa kasi ya kimbunga na kumkata mtama James ambaye bila kutarajia alijikuta chini karibu na beseni la moto. Alijikaza akainuka kwa kupepesuka ili kukabiliana na Jackline ambaye muda huo alikuwa kavimba akimsubiri ainuke ampe kichapo kingine.

Bahati haikuwa kwa James kwani alikutana na kichapo kingine na mbaya zaidi lile teke la mdomoni lilimpeleka chini tena James na kushuhudia meno kadhaa yakienda chini na kabla hajafanya chochote alimfuata na kumkaba na ile minyororo kiasi cha kuwafanya yale majitu kumrukia Jackline na kuanza kumtandika mangumi.

"Heeey kaa pembeni nani aliyewaambia huu ni ukumbi wa mapambano, haya bila shaka ulingo uko tayari twendeni nje tukashuhudie mpambano, wafungulie na hao wapuuzi wakashuhudie mwenzao akiagana na dunia."

Mzee Bruno alitamba. 

"Unafikiri nawaogopa twendeni fasta kabla shetani mnyonya damu hajatoka mwilini mwangu."

Jackline aliendelea kuwaduwaza mle ndani.

Walifunguliwa ile minyororo na wote wakatolewa nje mpaka kwenye eneo ambalo liliandaliwa kwa ajili ya pambano na kwa namna eneo lilivyokuwa liliashiria hapo hufanyika michezo kama hiyo kila wakati. Mzee Bruno alichukua kipaza na kutoa tangazo lililopenya kwenye kila sikio la aliyekuwa mle ndani.

"Watu wote mnatakiwa kufika kwenye machinjio kushuhudia mtu aliyechoka maisha akichinjwa kama kuku, wote acheni kazi zenu wahini ukingoni haraka."

Baada ya tangazo hilo kupita kila mmoja aliacha shughuli yake na kukimbilia eneo la tukio huku kila mmoja akijiuliza ni nani tena huyo aliyeamua kuchafua siku mle ngomeni.

" Kijana wangu hivi ni nani huyo aliyeamua kujitoa mhanga? "

Mzee mmoja aliyekuwa akifua vyuma alimuuliza kijana anayefanya naye kazi kule chini.

"Mzee wangu hata sijui ni nani mimi nadha twende tukashuhudie huko huko tutajua tukifika."

Watu zaidi ya mia tatu walikuwa wamelizunguka eneo la ulingo ambao ulikuwa umemwagwa tope ambalo kwa mtu asiyekuwa mzoefu nalo basi asingeweza kurusha hata teke moja kutokana na kuteleza. Miongoni mwao wakina Jasmine nao walikuwa karibu kabisa na ulingo chini ya ulinzi mkali huku wakimshuhudia Jackline alivyokuwa akijinyooshanyoosha kujiandaa na mpambano huo.

"Namuonea huruma Jackline kwa maamuzi aliyochukua sijui itakuwaje."

Jessica aliongea akiwa kashika shavu lake.

"Huyo ndiye Jackline mrembo wangu ambaye huwa akiamua jambo huwa harudi nyuma hata siku moja." Robinson alijibu huku akijifuta machozi.

Ndani ya ulingo mtu aliyekuwa akiingia kufungua mpambano hakuwa mwingine bali James ambaye alioshwa vya kutosha kule ndani. Na baada ya kuingia tu James kengele iligongwa na mpambano ulianza.

Jackline alikuwa ameshausoma ule ulingo hivyo alichokifanya ilikuwa ni kuruka juu na kumgonga kichwa kwa kiwiko na kumpeleka chini James na kisha Jackline alimfuata juu yake na kumnyonga kichwa. Tendo lile lilimshangaza sana mzee Bruno kwani kwa namna alivyoruka juu na kutua na kiwiko juu ya kichwa cha James hakutegemea kutokea.

"Mzee Bruno naomba nikwambie kitu, huu ni moto wa petroli ukigusa lazima uwake..."

"Weee kaa kimya hapo hujashinda kwa kumnyonga James, Brown muoneshe kazi huyo haraka."

Kama mshale Brown alitua ulingoni tayari kwa mpambano na baada ya filimbi tu, alimvamia Jackline miguuni na kumchota mzima mzima. Jackline aliangukia matope kwa kutanguliza mgongo.

" Yessss maliza kazi Brown, watu wote shangilieni kumpa nguvu kijana wetu."

Kweli shangwe liliongezeka na kumfanya Brown ahisi ameshinda mchezo alimfuata Jackline pale chini ili amuinue lakini hakujua kama ulikuwa mtego kwani alishtukia akipigwa teke la sehemu za siri.

" Ooishhhhh Mungu wangu weee nafwaaaaaa.... "

Brown alitoa kilio kwa maumivu makali aliyopata.

Na hapo hapo mzee Bruno aliinuka na kutoa tamko kali ambalo lilitokana na hasira baada ya watu wake wawili kupigwa na mwanamke hicho kilimkera sana Bruno.

"Askari mfunzeni adabu huyo ibilisi haraka."

"Ndiyo mkuu."

Askari kama nane waliingia ulingoni na kuanza kumshambulia kwa mafimbo yaliyotua kwenye kila kiungo cha Jackline, alijitahidi kujizuia lakini hakuweza kwani hawa walinzi walikuwa hawana chuguo la wapi wapige na hii ni kutokana na kifo cha kiongozi wao wa ulinzi bwana James Martin.

Hakika Jackline aliiva na ukizingatia lile eneo lilikuwa na matope usingeweza kumtambua Jackline aliyekuwa kama mfu hivi. Mwisho nguvu zilimwisha alianguka chini na kutulia kimya lakini juu yake kichapo kiliendelea. Hali hiyo iliinua hasira kwa Jasmine aliyepaza sauti yake.

"Mijanaume mizima msio na hata chembe ya huruma yaone, kama mna nguvu za kupambana si angeingia mmoja mmoja mbona mlimvamia na mafimbo? Si mngepanga mkono kama wenzenu? Mtu ameanguka bado mnaendelea kumshambulia tu nyinyi vipi? "

"Kweli, kweli, kweli...."

Sauti za wote waliojitokeza kushuhudia mpambano walipaza sauti zao kitendo ambacho kilimsimamisha mzee Bruno.

"Keleleeeeeee shwaini nyinyi nadhani mmenisahau eeehh."

"Wakukumbuke wewe kama nani bwana waache wapaze sauti zao mbona wakati Jackline akipigwa ulitoa amri washangilie vipi tena?"

Robinson aliinuka na kupaza sauti yake.

"Hee kila mtu aende sehemu yake ya kazi mara moja na ninyi walinzi peleka ndani hao pimbi kabla sijaamsha hasira zangu za urithi na huyo aliyeniulia kamanda wangu namsubiri si anajidai kafa tutaona."

Watu wote walikimbia kwenye maeneo yao kuendelea na shughuli zao huku wakina Jasmine wakirudishwa ndani na mara hii waliingizwa chumba kimoja wote pamoja na mgonjwa wao Jackline ambaye hatujui mzima au kafariki. Watu walikuwa wakiongea kila mmoja lake wengine wakimsifia Jackline kwa alichokifanya kwani haijawahi kutokea mmoja wa walinzi wa Ngome ile kuuawa mbele ya macho ya mzee Bruno na wengine walikuwa wakiwaonea huruma tu wakina Jasmine.

"Kale kadada kamenikumbusha mbali sana enzi zile naonesha video za kina Jetlee, Donnien ilikuwa shida mpaka mimi mwenyewe niliiga mapigo yake na baadaye kuanza kuyatumia mtaani, kuna siku niliotewa na mbishi mmoja aliyeingia bila kulipa kiingilio acha ndo hili pengo na mpaka leo sipendi ngumi ila kuangalia tu."

"Babu mimi nakupendeaga hapo tu kwenye saundi zako za uongo yaani umesahau kama hilo pengo ulipigwa ngumi na marehemu James ile siku ulipomtongoza mrembo wake Stella?"

"Haa hivi kweli eti na wewe hausahau tu, napo si kafa chezea kale kadada pigo moja tu mavi kuleee na sasa Stella wangu."

"Ninyi hapo bado mnashangaa nini potea?"

Mlinzi aliwatimua baada ya kuona wako bize na stori.


***


"Kijana habari yako." 

"Salama mzee shikamoo!" 

"Samahani naomba kuuliza." 

"Ndiyo uliza tu mzee wangu." 

"Sijui unamfahamu mzee fulani hivi anaitwa Fikirini?" 

"Ndiyo namfahamu vizuri sana." 

"Sijui unaweza kunipeleka kwake au kunielekeza kwake." 

"Hata kukupeleka pia naweza mzee." 

"Litakuwa jambo jema hilo kijana wangu." 

Basi yule kijana aliwapeleka moja kwa moja mpaka sehemu moja hivi karibu na makaburini kisha akamtaka asimamishe gari. 

"Kaka yangu bwana yaani aliamua kuja kuishi karibu na makaburini?"

Mzee Jonathan aliongea huku akionekana kushangaa. 

"Kwa maeneo ya vijijini haya mambo ya kawaida sana." 

Black alidakia naye. 

Muda huo wanatembea kuelekea eneo hilo la makaburi, yule kijana alikuwa anatuma ujumbe fulani sijui kwa nani. 

"MWENYEKITI KAMA AMBAVYO ULIAGIZA KUILINDA FAMILIA YA MZEE FIKIRINI TAYARI KUNA RASTA MMOJA YUKO WENZAKE WAWILI WANAMUULIZIA MAREHEMU MZEE FIKIRINI TUKO MAKABURINI NJOONI." 

"Kijana mbona hatufiki tu huko kwa mzee Fikirini?" 

Mzee Jonathan aliona aulize baada ya kuona wanazidi kuyakatisha tu makaburi. 

"Nataka tupitie huku nyumba yenyewe ni ile pale sasa njia ya kule juu imefungwa kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha zimepelekea korongo kubwa sana na hivyo kusababisha wakazi wa kieneo hiki kutumia hii njia ya makaburini." 

"Okay, ila hii mvua imekuja na majanga mengi sana sijui mpaka mwisho itakuwaje?" 

Black aliuliza baada ya kupata ufafanuzi kwanini walipita ile njia. 

"Nisubirini hapa kwanza nimgongee mlango."

Aliwataka wabaki pale nje ya fensi ya matete na kisha kijana huyo kuingia ndani ya ile nyumba. 

"Wenyewe mpo, wenyewe, wenyeweee, mzee nimekuletea wageni wako bwana."

Yule kijana aliongea hivyo kuwaaminisha wanaomsubiri kisha akazunguka nyuma ya ile nyumba na kukimbia. Wao Wakabaki pale wanasubiria. 

"Unajua nini taarifa ambazo nilipataga ni kwamba mzee huyu alifariki kipindi kidogo sasa mbona huyu dogo kasema yupo na huko ndani anaita jina hilo hilo la Mzee Fikirini." 

"Yawezekana ulidanganywa tu na aliyekupa taarifa." 

"Mmhh ni mtu niliyekuwa namuamini sana Black." 

"Amka mzee chini ya jua hakuna wa kuaminiwa hata mmoja." 

"We Black mbona kimya huko ndani hebu nenda kawaangalie bwana tunakwenda na muda eti." 

Black aliingia mpaka ndani lakini alishangaa kukuta kufuli mlangoni na nje kuna nguo tu kambani kuashiria 

kuwa wenyeji wapo lakini muda huo hawakuwepo. 

"Mzee huyu dogo hayupo huku ndani." 

"Whaaaaaat, unamaanisha nini Black? 


USIKOSE KATIKA SEHEMU INAYOFUATA KUJUA NINI KILIENDELEA. 


      #SULTANUWEZO

Sultan Uwezo

In our hands you will find out Songs and Videos of Various Artists without forgetting News from Newspapers. Here you will also find Employment's Information from the Government and the Private Sectors.

Post a Comment

Previous Post Next Post