REAL MADRID NA MANCHESTER CITY HAOO WATANGULIA ROBO FAINALI YA LIGI YA MABINGWA UEFA


MABINGWA watetezi, Manchester City wamefanikiwa kwenda hatua ya Robó Fainali Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya FC Copenhagen usiku wa jana Uwanja wa Etihad Jijini Manchester.
Mabao ya Manchester City yamefungwa na Manuel Akanji dakika ya tano, Julian Alvarez dakika ya tisa na Erling Haaland dakika ya 45 na ushei ambalo hilo linakuwa bao lake la 29 msimu huu huku bao la FC Copenhagen likifungwa na Mohamed Elyounoussi dakika ya 29.
Kwa matokeo hayo, Manchester City inakwenda Robo Fainali kwa ushindi wa jumla wa 6-2 kufuatia kuwachapa FC Copenhagen 3-1 pia kwenye mchezo wa kwanza Denmark.
Nao Real Madrid wametinga Robo Fainali pia licha ya kulazimishwa sare ya 1-1 na RB Leipzig jana Uwanja wa Santiago Bernabéu Jijini Madrid.
Vinícius Júnior alianza kuifungia Real Madrid dakika ya 65, kabla ya Vilmos Orbán kuisawazishia RB Leipzig dakika ya 68.
Real Madrid wanakwenda Robo Fainali kwa ushindi wa jumla wa 2-1 kufuatia kuwachapa RB Leipzig 1-0 kwenye mchezo wa kwanza Ujerumani.
Sultan Uwezo

In our hands you will find out Songs and Videos of Various Artists without forgetting News from Newspapers. Here you will also find Employment's Information from the Government and the Private Sectors.

Post a Comment

Previous Post Next Post